Changamoto Za Mtalaa Mpya Katika Ufundishaji Wa Lugha Ya Kiswahili Kwa Walimu Shule Za Upili, Wilayani Kasese.

Utafiti huu ulitazamia kushughulikia changamoto za mtalaa mpya katika ujifunzaji na ufundishaji wa lugha Kiswahili kwa walimu wa shule za upili wilayani kasese. Malengo ya utafiti huu yalikuwa kuchunguza changamoto za mtalaa mpya katika ufundishaji wa lugha ya Kiswahili, kutambua mabadiliko yaliyo...

Full description

Saved in:
Bibliographic Details
Main Author: Biira, Janet
Format: Thesis
Language:en_US
Published: Kabale University 2024
Subjects:
Online Access:http://hdl.handle.net/20.500.12493/2107
Tags: Add Tag
No Tags, Be the first to tag this record!
Description
Summary:Utafiti huu ulitazamia kushughulikia changamoto za mtalaa mpya katika ujifunzaji na ufundishaji wa lugha Kiswahili kwa walimu wa shule za upili wilayani kasese. Malengo ya utafiti huu yalikuwa kuchunguza changamoto za mtalaa mpya katika ufundishaji wa lugha ya Kiswahili, kutambua mabadiliko yaliyopo kati ya mtalaa mpya na mtalaa wa zamani, kuchunguza mikakati mbalimbali inayoweza kuwekwa ilikufanikisha ufundishaji wa lugha ya Kiswahili katika mtalaa wa mpya. Maswali ya utafiti huu yalikuwa; kwanza, mtalaa mpya unachangamoto zipi katika ufundishaji na ujiunzaji wa lugha ya kiswahi? Pili, je, kuna mabadiliko yoyote kati ya mtalaa mpya na mtalaa wa zamani? Tatu, ni mikakati ipi inayoweza kuwekwa ili kufanikisha ufundishaji wa na ujifunzaji wa wa lugha ya Kiswahili katika mtalaa mpya? Utafiti huu ulitumia utaratibu wa ukusanyaji data nyanjani au uwanjani kwa kutumia mbinu ya mahojiano. Vile vile, hojaji ilitumiwa (wanafunzi wa lugha ya Kiswahili). Mtafiti alitumia jumla ya shule sita mkiwemo shule ya upili ya Bwera, shule ya upili ya Karambi, shule ya upili ya St. Charles, shule ya upili ya Nyabugando Baptist, shule ya upili ya Hillside na ile ya Alliance zipatikanzo katika wilaya ya Kasese. Pia, mtafiti alitumia jumla ya shule sita za upili ambapo tatu zilikuwa ni za serekali na nyingine mbili ambazo ni za kibinafsi katika ukusanyaji wa data ya utafiti wake. Isitoshe, kutokana na matokeo ya utafiti huu yalidhihirisha kuwa kuwa kuna changamoto mbalimbali zilizotokana na mtalaa mpya mkiwemo; ukosefu wa vifaa vya kufundishia kama vitabu, upungufu wa vipindi vya Kiswahili, wanafunzi kulazimishwa kufanya miradi katika somo la Kiswahili na ukosefu wa walimu katika baadhi ya sehemu nchini Uganda. Pia utafiti huu kupitia data zake za uwanjani zilidhihirisha mabadiliko yafuatayo katika mtalaa mpya; kupunguka kwa vipindi, masomo yote kuchukua mfumo wa umilisi, wanafunzi kuchukua sehemu kubwa katika ufundishaji na ujifunzaji na kufanya miradi. Kuhusu mikakati ya kuweza kufanikisha ufundishaji katika mtalaa mpya hno ni kuwaruhusu wanafunzi kutumia Kiswahili katika mawasiliano yao ya kila siku, kutumia vifaa halisi na walimu kama vya kiteknolojia, kufundisha sarufi vilivyo. Mwisho kabisa, utafiti huu umetoa mapendekezo mbalimbali kwa walimu na wizara ya elimu kama kuongeza vipindi kwnye ratiba angalau vine kila wiki na kila kidato, wizara ya elimu kutoa vifaa vya kutosha vya kufundishia, wazazi na wakuu washule kuarifia kuhusu umuhimu/nafasi ya Kiswahili katika jumuiya Afrika Mashaariki, walimu kuongoza wanafunzi katika vipindi vya Kiswahili ipasavyo. Haya yakizingatiwa, yanaweza kuleta mabadiliko katika ufundishaji wa Kiswahili katika mtalaa mpya wa shule za upili.